Walioitwa Kwenye Usaili NFRA Septemba 2025

Bonyeza KUJIUNGA NASI WHATSAPP Kwa nafasi za kazi, matangazo mbalimbali Ajira mpya kutoka Serikalini, Kampuni, Taasisi mbalimbali TAESA, Viwandani, Internships.

Hili hapa tangazo na orodha ya majina ya walioitwa kwenye usaili Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula (NFRA) anapenda kuwataarifu Waombaji Kazi kuwa usaili unatarajiwa kuendeshwa kuanzia tarehe 01 Septemba, 2025 hadi 04 Septemba, 2025 na hatimaye kuwapangia vituo vya kazi waombaji kazi watakaofaulu usaili huo.

Wasailiwa wanaoitwa kwenye usaili wanapaswa kuzingatia maelekezo yafuatayo:

  1. Usaili utafanyika kuanzia tarehe kama ilivyooneshwa kwenye tangazo hili, muda na sehemu ambapo usaili utafanyika umeainishwa kwa kila Kada.
  2. Kila msailiwa anapaswa kuwa na kitambulisho kwa ajili ya utambuzi.
  3. Vitambulisho vinavyokubalika ni pamoja na: Kitambulisho cha Mzanzibari Mkazi, Kitambulisho cha Mpiga kura, Kitambulisho cha kazi, Kitambulisho cha Uraia, Hati ya kusafiria, Leseni ya Udereva au barua ya utambulisho kutoka Serikali ya Mtaa/Kijiji unachotoka.
  4. Wasailiwa wanatakiwa kufika na vyeti vyao halisi, kuanzia cheti cha kuzaliwa, kidato cha IV, VI, Astashahada, Stashahada, Stashahada ya Juu, Shahada na kuendelea kutegemeana na sifa za mwombaji.
  5. Wasailiwa watakaowasilisha Testimonials, Provisional Results, Statement of Results, au hati za matokeo za kidato cha IV na VI hawatakubalika na hawataruhusiwa kuendelea na usaili.
  6. Kila msailiwa atajigharamia kwa chakula, usafiri na malazi.
  7. Kila msailiwa azingatie tarehe, muda na mahali alipopangiwa kufanyia usaili.
  8. Kwa waombaji waliosoma nje ya Tanzania wahakikishe vyeti vyao vimehakikiwa na kuidhinishwa na mamlaka husika (TCU, NACTVET au NECTA).
  9. Kwa kada ambazo zinahitaji usajili na bodi zao za kitaaluma, waombaji wanapaswa kuja na vyeti vyao halisi vya usajili pamoja na leseni halali za kufanyia kazi.
  10. Wasailiwa ambao majina yao yanatofautiana katika nyaraka zao wanapaswa kuwasilisha hati ya kiapo cha kubadili jina (Deed Poll) iliyosajiliwa na Wizara ya Ardhi.

Ratiba ya Usaili NFRA

1. UsaIli wa Maandishi – 01/09/2025

Mahali: Chuo Kikuu Kishiriki cha Elimu Dar es Salaam (DUCE)
Muda: Saa 1:00 Asubuhi

Na.Kada
1Afisa Hesabu II
2Afisa Hesabu Msaidizi II
3Afisa Kilimo Msaidizi II
4Afisa Masoko II
5Afisa TEHAMA II
6Afisa Utumishi II
7Mhandisi II
8Msaidizi wa Kumbukumbu II
9Mchumi II
10Afisa Ugavi II
11Afisa Ugavi Msaidizi II
12Fundi Sanifu II

2. UsaIli kwa Vitendo

Na.KadaTareheMahaliMuda
1Dereva II01/09/2025VETA – Chang’ombe, Dar es SalaamSaa 1:00 Asubuhi
2Mwandishi/Mwendesha Ofisi II01/09/2025Ofisi za NFRA – Chang’ombe, Dar es SalaamSaa 1:00 Asubuhi
3Fundi Sanifu II02/09/2025VETA – Chang’ombe, Dar es SalaamSaa 1:00 Asubuhi

3. UsaIli wa Mahojiano – 04/09/2025

Mahali: Chuo cha Bandari
Muda: Saa 1:00 Asubuhi

Na.Kada
1Afisa Hesabu II
2Afisa Hesabu Msaidizi II
3Afisa Kilimo Msaidizi II
4Afisa Masoko II
5Afisa Sheria II
6Afisa TEHAMA II
7Afisa Utumishi II
8Dereva II
9Mhandisi II
10Mhasibu II
11Msaidizi wa Kumbukumbu II
12Mwandishi/Mwendesha Ofisi II
13Fundi Sanifu II
14Mchumi II
15Afisa Ugavi II
16Afisa Ugavi Msaidizi I

Pakua PDF ya majina hapa.

Soma zaidi: