Haya hapa majina ya wananafunzi Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi (MoCU) kinapenda kuwataarifu waombaji wote walioomba nafasi ya kujiunga na programu mbalimbali kupitia TAMISEMI, kuwa majina ya waliochaguliwa kwa mwaka wa masomo 2025/2026 yametolewa rasmi.
Jinsi ya Kuangalia Majina na Kupakua fomu ya kujiunga
Waombaji wote wanashauriwa kutembelea tovuti rasmi ya MoCU kupitia kiungo:
- Kupitia tovuti maalumu ya chuo https://www.mocu.ac.tz
- Pakua PDF hapa ya majina
Kisha, fuata maelekezo haya:
- Jina la Mtumiaji (Username): Tumia namba yako ya mtihani wa kidato cha nne (Mfano: S0000-0000-2024)
- Nywila (Password): Tumia jina lako la mwisho lililoandikwa kwa herufi kubwa
Baada ya kuingia, utaweza kupakua barua ya kudahiliwa (Admission Letter) pamoja na fomu ya maelekezo ya kujiunga (Joining Instructions Form).
Maelezo Muhimu Kuhusu MoCU
MoCU ni chuo kinachotoa elimu bora katika masuala ya ushirika, biashara, teknolojia ya habari, na maendeleo ya vijijini. Makao makuu yake yapo Moshi Mjini, mkoa wa Kilimanjaro, katika barabara ya Sokoine, chini ya Mlima Kilimanjaro. Pia kina matawi na ofisi 13 za kikanda zinazohudumia mikoa yote ya Tanzania.
Kwa Mawasiliano Zaidi
Unaweza kupiga simu kupitia namba zifuatazo kwa msaada au maelekezo zaidi:
- 0738 568 023
- 0738 568 024
- 0738 568 025
- 0617 474 711
- 0772 674 711
Soma zaidi:
Leave a Reply
View Comments