Angalia hapa orodha ya majina walioitwa kwenye usaili Tume ya Utumishi wa Mahakama 2025-26 PDF inapenda kuwafahamisha waombaji wote wa ajira walioomba nafasi mbalimbali zilizotangazwa tarehe 3 Juni 2025 kuwa, baada ya uchambuzi wa maombi, baadhi ya waombaji wamechaguliwa kushiriki kwenye usaili wa hatua ya kwanza.
Ratiba ya Usaili wa Awali – Julai 2025
Majina ya walioitwa kwenye usaili huo pamoja na tarehe, muda na vituo vya usaili yameorodheshwa katika orodha rasmi iliyowekwa kupitia tovuti ya Tume: www.jsc.go.tz.
Muhimu kufuatwa:
- Kila msailiwa anafanya usaili katika kituo alichopangiwa tu – hakutakuwa na mabadiliko ya vituo.
- Usaili huu utafanyika kwa njia ya Kielektroniki (Computer Based Interview).
- Wasailiwa wote wanatakiwa kufika na:
- Kitambulisho cha Taifa (NIDA)
- Vyeti halisi vya taaluma (Academic Certificates)
- Vyeti vya sekondari (O-level/A-level)
Waombaji watakaofaulu hatua ya kwanza, watajulishwa kuhusu hatua inayofuata, ambayo ni usaili wa kujieleza (Oral Interview) na/au Vitendo (Practical Interview) kupitia tovuti ya Tume.
Kwa waombaji ambao hawajaona majina yao, wafahamu kuwa hawakufanikiwa kufuzu kwa hatua ya usaili wa awali.
Ratiba ya Usaili wa Awali Tume ya Mahakama Julai 2025
| Na. | Tarehe | Siku | Kada Zilizoitwa |
|---|---|---|---|
| 1 | 19 Julai 2025 | Jumamosi | Msaidizi wa Kumbukumbu |
| 2 | 21 Julai 2025 | Jumatatu | Afisa Mwongoza Ofisi, Mwandishi, Mkutubi, Msaidizi wa Maktaba |
| 3 | 22 Julai 2025 | Jumanne | Wataalamu wa Ufundi: Umeme, Bomba, Uchoraji, Useremala, Uchomeleaji, Friji |
| 4 | 23 Julai 2025 | Jumatano | Hakimu Mkazi, Mpishi, Msaidizi wa Hesabu |
| 5 | 24 Julai 2025 | Alhamisi | Opereta wa Kompyuta, Opereta Msaidizi, Dereva |
| 6 | 25 Julai 2025 | Ijumaa | Mlinzi, Msaidizi wa Ofisi |
| 7 | 26 Julai 2025 | Jumamosi | Afisa Utumishi |
Maelezo Zaidi na Mawasiliano:
Tembelea tovuti rasmi: www.jsc.go.tz
Simu: 0734 219 821 au 0738 247 341
Barua pepe: maulizo.ajira@jsc.go.tz
Soma zaidi:
- Chuo cha Makumira Training Institute (MTI)
- Orodha ya Waliochaguliwa UDOM 2025-26 PDF
- Chuo cha Simiyu College of Health and Allied Sciences
- Mfumo wa Maombi ya Ajira kwa Walimu Mtandaoni
Imetolewa na:
Lydia Churi
Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
Tume ya Utumishi wa Mahakama
Leave a Reply
View Comments