Orodha ya Waliochaguliwa Kujiunga na Chuo zaidi ya Kimoja TCU 2025 PDF

Bonyeza KUJIUNGA NASI WHATSAPP Kwa nafasi za kazi, matangazo mbalimbali Ajira mpya kutoka Serikalini, Kampuni, Taasisi mbalimbali TAESA, Viwandani, Internships.

Hii haoa orodha ya majina ya waliochaguliwa kujiunga na chuo zaidi ya kimoja PDF Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU) inaufahamisha umma kuwa Awamu ya Kwanza ya udahili wa Shahada ya Kwanza kwa mwaka wa masomo 2025/2026 imekamilika. Jumla ya waombaji na nafasi zilikuwa kama ifuatavyo:

Angalia hapa majina ya waliochaguliwa TCU pdf.

Orodha ya Waombaji waliodahiliwa zaidi ya Chuo kimoja au Programu zaidi ya moja hii hapa PDF ya majina.

Waliochaguliwa Kujiunga na Vyuo

KigezoTakwimu 2025/2026Kumbukumbu 2024/2025Tofauti
Idadi ya waombaji146,879
Idadi ya vyuo vilivyoruhusiwa88
Idadi ya programu894856+38
Nafasi za udahili205,652198,986+6,666 (3.3%)
Waombaji waliodahiliwa116,596 (79.4%)

Waombaji Waliodahiliwa Zaidi ya Chuo Kimoja

Waombaji waliopata nafasi katika zaidi ya chuo kimoja wanapaswa:

  • Kuthibitisha udahili wao katika chuo kimoja pekee kati ya tarehe 03 – 21 Septemba 2025.
  • Uthibitisho unafanyika kwa kutumia namba ya siri (confirmation code) iliyotumwa kwa SMS au barua pepe.
  • Wale ambao hawajapokea ujumbe wanashauriwa kuingia kwenye mifumo ya vyuo walivyodahiliwa na kuomba kutumiwa namba ya uthibitisho.
  • Orodha ya majina ya waliodahiliwa zaidi ya chuo kimoja inapatikana katika tovuti ya TCU: www.tcu.go.tz.

Awamu ya Pili ya Udahili

TCU inatangaza kufunguliwa kwa Awamu ya Pili ya Udahili kuanzia 03 – 21 Septemba 2025.

Fursa hii ni kwa:

  • Waombaji ambao hawakuwasilisha maombi kwenye Awamu ya Kwanza.
  • Waombaji ambao hawakupata nafasi ya kudahiliwa kutokana na ushindani.

Maelekezo:

  • Vyuo vya Elimu ya Juu vimetakiwa kutangaza programu ambazo bado zina nafasi.
  • Waombaji wanashauriwa kuzingatia ratiba na taratibu zilizowekwa kwenye kalenda ya udahili kupitia tovuti ya TCU (www.tcu.go.tz).

Wito kwa Waombaji

  • Waombaji wanakumbushwa kuwa masuala yote ya udahili au uthibitisho yawasilishwe moja kwa moja kwenye vyuo husika.
  • Vyuo vimeelekezwa kutoa msaada wa haraka kwa wanafunzi watakaokutana na changamoto za kiufundi.

Soma zaidi: