Nafasi za Mafunzo ya Ualimu Wizara ya Elimu (WyEST)

Bonyeza KUJIUNGA NASI WHATSAPP Kwa nafasi za kazi, matangazo mbalimbali Ajira mpya kutoka Serikalini, Kampuni, Taasisi mbalimbali TAESA, Viwandani, Internships.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia anatangaza nafasi za kujiunga na Mafunzo ya Stashahada ya Ualimu katika fani zifuatazo:

  1. Stashahada ya Ualimu Elimu ya Awali – Miaka 2
  2. Stashahada ya Ualimu Elimu ya Msingi – Miaka 2
  3. Stashahada ya Ualimu Elimu Maalumu – Miaka 2
  4. Stashahada Maalumu ya Ualimu Elimu ya Msingi (Sayansi na Hisabati) – Miaka 3

Mafunzo yatatolewa katika Vyuo vya Ualimu vya Serikali na visivyo vya Serikali.

Sifa za Kujiunga

A. Stashahada ya Ualimu Elimu ya Awali/Msingi/Maalumu (Miaka 2)

  • Wahitimu wa Kidato cha Sita wenye ufaulu wa Daraja la I–III na Principal Pass mbili (02).
  • Waliosoma Economics, Commerce au Book Keeping waombe kozi ya Elimu ya Awali.
  • Walimu wenye Cheti cha Ualimu wa Elimu ya Awali au Msingi pia wanaruhusiwa kuomba.

B. Stashahada Maalumu ya Ualimu Elimu ya Msingi – Sayansi & Hisabati (Miaka 3)

  • Wahitimu wa Kidato cha Nne wenye ufaulu wa Daraja la I–III.
  • Wenye alama C au zaidi katika masomo matatu, na mawili kati ya haya:
    • Basic Mathematics
    • Biology
    • Chemistry
    • Physics
    • Information and Computer Studies
    • Computer Science

Vyuo na Aina ya Mafunzo

Jedwali la vyuo na kozi husika limeambatanishwa na tangazo hili kwenye tovuti ya Wizara.

Maelekezo ya Maombi

  • Maombi yafanywe kwa kuzingatia sifa zilizotajwa.
  • Mafunzo yatatolewa na vyuo vya Serikali na visivyo vya Serikali vilivyoteuliwa na Wizara.

Soma zaidi: