Nafasi za Kazi Wilaya ya Wanging’ombe

Bonyeza KUJIUNGA NASI WHATSAPP Kwa nafasi za kazi, matangazo mbalimbali Ajira mpya kutoka Serikalini, Kampuni, Taasisi mbalimbali TAESA, Viwandani, Internships.

Hili hapa tangazo la nafasi za kazi Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Wanging’ombe anatangaza nafasi za kazi zilizotokana na kibali cha ajira kipya chenye Kumb. Na. FA.97/228/01/A/25 cha tarehe 29/04/2025 kutoka Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora.

Waombaji wenye sifa wanakaribishwa kuomba nafasi kama zilivyoainishwa hapa chini:

Ajira mpya zilizotangazwa na Maelezo

Kada ya KaziIdadi ya NafasiSifa za MwombajiNgazi ya Mshahara
Msaidizi wa Kumbukumbu Daraja II4– Elimu ya Kidato cha IV/VI- Stashahada (Diploma NTA Level 6) ya Masjala kutoka chuo kinachotambuliwa na Serikali- Ujuzi wa kompyutaTGS C1
Mwandishi Mwendesha Ofisi Daraja II5– Elimu ya Kidato cha IV/VI- Diploma ya Uhazili au Cheti cha NTA Level 6- Uwezo wa hatimkato maneno 100/min (Kiswahili & Kiingereza)- Ujuzi wa programu za ofisi (Word, Excel, PowerPoint, Internet, Email, Publisher)TGS C1
Dereva Daraja II13– Elimu ya Kidato cha IV/VI- Leseni daraja E au C yenye uzoefu ≥ mwaka 1 bila kusababisha ajali- Cheti cha Basic Driving Course (VETA au chuo kinachotambuliwa na Serikali)TGS B1
Muhudumu wa Boti (Deckhand Auxiliaries)1– Elimu ya Kidato cha IV- Cheti cha Teknolojia ya Uvuvi (FETA) au Cheti cha Uhudumu wa Meli (DMI) au sifa inayolingana kutoka chuo kinachotambuliwa na SerikaliTGOS A

Masharti ya Jumla:

  1. Mwombaji awe raia wa Tanzania mwenye umri kuanzia miaka 18 na usiozidi 45.
  2. Wenye ulemavu wanahamasishwa kuomba na waeleze aina ya ulemavu kwenye mfumo wa maombi.
  3. Waambatishe wasifu binafsi (CV) yenye mawasiliano na majina ya wadhamini watatu.
  4. Vyeti vyote vya elimu na taaluma viwe vimeidhinishwa na Mwanasheria/Wakili.
  5. Vyeti vya provisional results, statement of results na result slips (Form IV & VI) havikubaliki.
  6. Waombaji wa kada ya dereva waambatishe vyeti vya mafunzo ya udereva.
  7. Waombaji waliostaafu Utumishi wa Umma hawaruhusiwi kuomba isipokuwa kwa kibali cha Katibu Mkuu Kiongozi.
  8. Vyeti vya nje ya nchi viwe vimehakikiwa na mamlaka husika (TCU, NECTA, NACTVET).
  9. Taarifa za kughushi hazitakubalika na hatua kali za kisheria zitachukuliwa.

Jinsi ya Kutuma Maombi

Barua ya maombi ielekezwe kwa:

Mkurugenzi Mtendaji
Halmashauri ya Wilaya ya Wanging’ombe
S.L.P. 64,
Njombe.

Mwisho wa kutuma maombi: 01 Septemba, 2025

Soma zaidi: