Hili hapa tangazo la nafasi za kazi Wilaya ya Songwe Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Songwe amepokea kibali cha Ajira mpya kwa ikama ya mwaka 2024/2025 kutoka kwa Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora chenye Kumb. Na.FA.97/228/01/A/25 ya tarehe 29/04/2025. Hivyo Watanzania wote wenye sifa wanatangaziwa kutuma maombi ya kazi kwa nafasi zifuatazo: –
Ajira mpya zilizotangazwa na Maelezo
1. Dereva Daraja la II – Nafasi 4
Sifa za Mwombaji:
- Awe Mtanzania mwenye umri kati ya miaka 18 hadi 45
- Awe na cheti cha Kidato cha Nne (Form IV)
- Awe na leseni ya daraja E au C aliyofanyia kazi kwa muda usiopungua mwaka mmoja bila kusababisha ajali
- Awe amehitimu mafunzo ya msingi ya udereva (Basic Driving Course) kutoka VETA au chuo kinachotambuliwa na Serikali
Majukumu ya Kazi:
- Kukagua gari kabla na baada ya safari ili kuhakikisha usalama
- Kuwasafirisha watumishi katika safari za kikazi
- Kufanya matengenezo madogo madogo ya gari
Ngazi ya Mshahara:
Kwa kuzingatia ngazi ya Mishahara ya Serikali – TGS B
Maelekezo kwa Waombaji:
- Maombi yaambatane na barua ya maombi ya kazi iliyosainiwa na vyeti vifuatavyo:
- Cheti cha kuzaliwa
- Cheti cha Kidato cha Nne (Form IV)
- Leseni ya udereva ya daraja E au C
- Cheti cha mafunzo ya udereva kutoka VETA au chuo kinachotambuliwa
- Wasifu binafsi (CV) unaoonesha anuani ya sasa, namba ya simu na barua pepe
- Majina ya wadhamini (referees) watatu wa kuaminika
- Waombaji waliosoma nje ya nchi wahakikishe vyeti vyao vimehakikiwa na kuidhinishwa na mamlaka husika (NECTA, NACTE, au TCU)
- Maombi yasiyoambatishwa na vyeti halisi yaliyoidhinishwa na wakili hayatafanyiwa kazi
- Hatutapokea “testmonial”, “statement of results”, au “result slip” kwa Kidato cha Nne au Sita
- Waombaji waliostaafu katika utumishi wa umma hawaruhusiwi kuomba isipokuwa kwa kibali cha Katibu Mkuu Kiongozi
- Taarifa za kughushi zitachukuliwa hatua za kisheria
Jinsi ya kutuma maombi
Maombi yote yatumwe kwa njia ya mtandao kupitia mfumo wa Recruitment Portal:
https://portal.ajira.go.tz
(Pitia sehemu iliyoandikwa “Recruitment Portal”)
Anwani ya Barua:
Mkurugenzi Mtendaji
Halmashauri ya Wilaya ya Songwe
S.L.P 77,
SONGWE
Mwisho wa kutuma maombi ni tarehe 19 Agosti, 2025.
Wahitimu wote wenye sifa wanahimizwa kutuma maombi kwa wakati.
Read also:
Leave a Reply
View Comments