Nafasi za Kazi Wilaya ya Kasulu

Bonyeza KUJIUNGA NASI WHATSAPP Kwa nafasi za kazi, matangazo mbalimbali Ajira mpya kutoka Serikalini, Kampuni, Taasisi mbalimbali TAESA, Viwandani, Internships.

Hili hapa tangazo la nafasi za kazi Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kasulu anawaalika Watanzania wenye sifa kuomba ajira mpya na mbadala zilizopatikana kwa mwaka wa fedha 2023/2024 na 2024/2025 kupitia vibali rasmi kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora.

Nafasi Zinazotangazwa

1. Mwandishi Mwendesha Ofisi Daraja II – Nafasi 12

Majukumu:

  • Kuchapa barua na nyaraka (za kawaida na za siri)
  • Kupokea wageni na kuwaelekeza
  • Kutunza kumbukumbu za ratiba, vikao, safari

Sifa za Mwombaji:

  • Elimu ya Kidato cha IV au VI
  • Stashahada ya Uhazili au Cheti cha NTA Level 6

Mshahara: TGS C

2. Dereva Daraja II – Nafasi 3

Majukumu:

  • Kukagua gari kabla/baada ya safari
  • Kuwasafirisha watumishi kikazi

Sifa za Mwombaji:

  • Kidato cha IV na cheti cha mtihani
  • Leseni ya Daraja “E” au “C”

Mshahara: TGS B

Masharti ya Jumla kwa Waombaji

  • Raia wa Tanzania, umri miaka 18 hadi 45
  • Wenye ulemavu wanahimizwa kuomba na kutaja aina ya ulemavu
  • Waambatishe cheti cha kuzaliwa kilichothibitishwa na wakili
  • Waajiriwa wa umma kwenye nafasi za kuingilia hawaruhusiwi kuomba
  • Ambatishe CV, namba za simu na wadhamini 3
  • Vyeti vya taaluma (Kidato cha IV, VI, taaluma husika) vithibitishwe na wakili

Tarehe ya Mwisho na Namna ya Kutuma Maombi

Mwisho wa kutuma maombi: 14/08/2025

Anuani ya Barua:
Mkurugenzi Mtendaji,
Halmashauri ya Wilaya ya Kasulu,
S.L.P 97,
Kasulu.

Tuma Maombi Kupitia:
https://portal.ajira.go.tz

Maombi yasiyowasilishwa kwa njia hii hayatapokelewa.

Soma zaidi: