Nafasi za Kazi Wilaya ya Kaliua

Bonyeza KUJIUNGA NASI WHATSAPP Kwa nafasi za kazi, matangazo mbalimbali Ajira mpya kutoka Serikalini, Kampuni, Taasisi mbalimbali TAESA, Viwandani, Internships.

Hili hapa tangazo la nafasi za kazi Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kaliua, kupitia kibali kutoka Ofisi ya Rais – Utumishi, anakaribisha maombi ya kazi kutoka kwa Watanzania wenye sifa stahiki kujaza nafasi mbalimbali kama ifuatavyo:

Ajira mpya zilizotangazwa na Maelezo

1. Msaidizi wa Kumbukumbu Daraja la II – Nafasi 4

Sifa:

  • Elimu ya kidato cha Nne au Sita
  • Stashahada (Diploma – NTA Level 6) ya Utunzaji wa Kumbukumbu kutoka chuo kinachotambuliwa na Serikali
  • Uwezo wa kutumia kompyuta

Majukumu:

  • Kuorodhesha barua zinazoingia na kutoka
  • Kusambaza na kurudisha majalada
  • Kufuatilia mzunguko wa majalada katika ofisi

Mshahara: TGS C

2. Dereva Daraja la II – Nafasi 3

Sifa:

  • Cheti cha Kidato cha Nne
  • Leseni ya daraja E au C, na uzoefu wa angalau mwaka 1 bila kusababisha ajali
  • Vyeti vya mafunzo ya udereva kutoka VETA au chuo kinachotambulika na Serikali

Majukumu:

  • Kukagua gari kabla/baada ya safari
  • Kuwapeleka watumishi katika safari za kikazi
  • Matengenezo madogo madogo na kutunza “logbook”
  • Kusambaza nyaraka na kufanya usafi wa gari

Mshahara: TGS B

Masharti ya Jumla kwa Waombaji:

  • Umri miaka 18 – 45
  • Raia wa Tanzania
  • Vyeti vya elimu na taaluma viwe vimehakikiwa na kuidhinishwa na mwanasheria/wakili
  • Testimonials, Statement of Results, au Provisional Results hazitakubalika
  • Waombaji wenye ulemavu wanahamasishwa kutuma maombi
  • Vyeti vya nje ya Tanzania viwe vimehakikiwa na TCU, NECTA au NACTVET
  • Waombaji waliostaafu au walioko tayari kazini Serikalini hawapaswi kuomba (isipokuwa kwa kibali maalum)

Jinsi ya Kutuma Maombi

Maombi yote yatume kupitia mfumo wa ajira wa Serikali:
https://portal.ajira.go.tz
Mwisho wa kutuma maombi: 14 Agosti, 2025

Anuani ya barua ya maombi:
Halmashauri ya Wilaya ya Kaliua,
S.L.P 83
KALIUA

Maombi yasiyotumwa kwa mfumo huu hayatafanyiwa kazi.

Soma zaidi: