Nafasi za Kazi Wilaya ya Iringa

Bonyeza KUJIUNGA NASI WHATSAPP Kwa nafasi za kazi, matangazo mbalimbali Ajira mpya kutoka Serikalini, Kampuni, Taasisi mbalimbali TAESA, Viwandani, Internships.

Hili hapa tangazo la nafasi za kazi Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa amepokea kibali cha ajira mpya kutoka kwa Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais – Utumishi chenye Kumb. Na. FA. 97/228/01/A/25 cha tarehe 29 Aprili, 2025. Hivyo, anakaribisha maombi ya kazi kutoka kwa Watanzania wenye sifa za kujaza nafasi zifuatazo:

Ajira mpya zilizotangazwa na Maelezo

1. Dereva Daraja la II – Nafasi 05

Majukumu:

  • Kukagua gari kabla na baada ya safari
  • Kuwapeleka watumishi safari za kikazi
  • Kufanya matengenezo madogo ya gari

Sifa:

  • Cheti cha Kidato cha Nne
  • Leseni ya Daraja E au C
  • Uzoefu wa mwaka 1 bila kusababisha ajali
  • Cheti cha mafunzo ya udereva kutoka VETA au chuo kinachotambuliwa na Serikali

Mshahara: TGS B1

2. Msaidizi wa Kumbukumbu Daraja la II – Nafasi 04

Majukumu:

  • Kuorodhesha barua zinazoingia na kutoka
  • Kusambaza majalada kwa watendaji

Sifa:

  • Kidato cha Nne au Sita
  • Diploma ya Utunzaji Kumbukumbu (NTA level 6)
  • Ujuzi wa kompyuta

Mshahara: TGS C

3. Mwandishi Mwendesha Ofisi Daraja la II – Nafasi 05

Majukumu:

  • Kuchapa nyaraka za kawaida na za siri
  • Kupokea wageni na kuwaelekeza

Sifa:

  • Kidato cha Nne/Sita
  • Diploma ya Uhazili au NTA level 6 ya uandishi
  • Hatimkato ya Kiswahili & Kiingereza (maneno 100 kwa dakika)
  • Ujuzi wa programu za ofisi: Word, Excel, PowerPoint, Internet, Email, Publisher

Mshahara: TGS C

Masharti ya Jumla kwa Waombaji:

  • Awe Raia wa Tanzania mwenye umri miaka 18 hadi 45
  • Waombaji wenye ulemavu wanahimizwa kutuma maombi
  • Ambatanisha CV yenye maelezo kamili, namba ya simu, email, na majina ya wadhamini 3
  • Ambatanisha vyeti halisi vilivyothibitishwa na Mwanasheria/Wakili (Form IV, VI, Diploma n.k.)
  • Statement of results au result slips hazikubaliki
  • Aliyesoma nje ya nchi, vyeti viwe vimehakikiwa na NECTA/NACTVET/TCU
  • Aliyestaafu utumishi wa umma haruhusiwi kuomba bila kibali cha Katibu Mkuu Kiongozi
  • Vyeti vya mafunzo ya udereva ni lazima kwa waombaji wa nafasi ya dereva
  • Usitumie taarifa za kughushi – hatua za kisheria zitachukuliwa
  • Barua ya maombi lazima isainiwe na ielekezwe kwa:

Jinsi ya kutuma maombi

Maombi yote yatumwe kwa njia ya mtandao kupitia mfumo wa Ajira:
https://portal.ajira.go.tz

Mwisho wa kutuma maombi: 14 Agosti, 2025.

Mkurugenzi Mtendaji,
Halmashauri ya Wilaya ya Iringa,
12 Njia Panda ya Mgama,
S.L.P. 108,
IRINGA.

Soma zaidi: