Nafasi za Kazi 70 Unitrans Tanzania Ltd

Bonyeza KUJIUNGA NASI WHATSAPP Kwa nafasi za kazi, matangazo mbalimbali Ajira mpya kutoka Serikalini, Kampuni, Taasisi mbalimbali TAESA, Viwandani, Internships.

Nafasi za kazi Kampuni ya Unitrans Tanzania Ltd ya jijini Dar es Salaam inatangaza nafasi za ajira kwa vijana 70 wa kiume na wa kike kama Madereva.

Nafasi: Madereva wa Malori (Truck Drivers) – 70 nafasi
Eneo la kazi: Kilombero
Aina ya Mkataba: Msimu (Seasonal)

Soma: Jinsi ya kuangalia Matokeo ya Darasa la Saba 2025 PSLE 2025/26

Majukumu:

  • Kusafirisha miwa kutoka mashambani hadi kiwandani.
  • Kufanya kazi nyingine zinazohusiana na udereva zitakazopangwa.

Sifa za Mwombaji

  • Awe na uelewa wa sheria na kanuni za usalama barabarani.
  • Awe na leseni halali ya daraja E.
  • Awe na uwezo wa kusoma na kuandika.
  • Awe na cheti cha udereva wa magari makubwa (Rigid/HGV) kutoka chuo kinachotambulika na serikali.
  • Awe na uzoefu wa angalau miaka 2 katika kuendesha malori.
  • Umri kati ya miaka 25 – 45.
  • Uwezo na utayari wa kufanya kazi usiku.
  • Awe na barua ya uthibitisho wa leseni kutoka Jeshi la Polisi Tanzania.

Jinsi ya Kuomba

Wakilishi wanatakiwa kuwasilisha:

  • Barua ya maombi
  • Wasifu binafsi (CV)
  • Nakala za vyeti husika
  • Nakala ya cheti cha TIN
  • Nakala ya kitambulisho cha NIDA

Anuani ya kutuma maombi:

Human Resources Manager
Unitrans Tanzania Ltd
P.O. Box 50, Kidatu

Au kwa barua pepe: iness.nangali@unitrans.co.tz

Mwisho wa kutuma maombi: 30 Septemba 2025.

Soma zaidi: